Friday 10 November 2017

CHANGAMOTO ZA WAIMBAJI WA KIKE WA NYIMBO ZA INJILI


Kumekuwa na wimbi kubwa sana la waimbaji wakike wa nyimbo za injili,kila siku kwa wastani kuna waimbaji kumi wapya kabisa wanatambulishwa kwa njia mbalimbali aidha redioni,kwenye tv,magazetini,majaridani hata mitandaoni.
Wimbi hili la ongezeko la waimbaji wa kike haliendani na utoaji wa albamu. Katika hili kuna mijadala mbalimbali juu ya kwanini waimbaji wa kike wengi hawatoi albamu zao na hizi ndio baadhi ya sababu zinazochangia:

Saturday 23 January 2016

UNAITWA,TUPA VAZI LAKO


MARKO 10;46-52
Inaelezea kulikuwa na Bartimayo kipofu alikuwa amekaa chini kando ya njia hajui maisha yake yatakuwaje,anavizia watu waje wamsaidie amekuwa ombaomba kwa miaka mingi kutokana na upofu wake,inawezekana nawe una upofu wa ndani umeteseka kwa jambo Fulani kwa miaka mingi hujui utatokaje hapo ktk magumu yako..YESU alipopita Bartimayo hakulaza damu akaanza kupaza sauti akimwita YESU...
Mstari 48-50. Na wengi wakamkemea ili anyamaze, lakini alizidi kupaza sauti, Mwana wa Daudi, unirehemu.Yesu akasimama akasema, Mwiteni. Wakamwita yule kipofu, wakamwambia, Jipe moyo; inuka, anakuita.AKATUPA VAZI

NAMNA YA KUWATAMBUA MANABII WA UONGO.

Bwana Yesu alishatuonya tujihadhari na manabii wa uongo na tena akawafananisha na mbwa mwitu wakali waliovaa ngozi ya kondoo (Math 7:15-23). Yesu alibainisha wazi kuwa namna pekee ya kuwatambua ni kuyachunguza matunda yao..Lakini mtume Petro amerahisisha zaidi kwa kufafanua tabia zao ktk 2Pet 2:1-22.,Nazo ni...

HASARA ZA KUFANYA NGONO KABLA YA NDOA.

Nimeitoa mahali naamini itakusaidia kijana
Andiko la Msingi ni Mithali 5:1-20
"Mungu ndiye aliyewaumba mtu mume na mtu mke, akawaweka bustanini ili wamtumikie. Mungu akamuumba mwanadamu na kumpa viungo mbalimbali katika mwili. Akawapa wanadamu maungo maalumu kwa ajili ya tendo la ndoa na kisha akaliweka tendo la ndoa kuwa takatifu, tena la halali kwa wanandoa tu, tena hasa wale waliounganishwa na yeye."
Sasa katika kizazi cha leo tunaona watu wengi hasa vijana ambao bado hawajaoana (kwa maana ya kuwa wanandoa) vijana hao wanafanya tendo hilo la ndoa (ngono) tena kwa uchafu usio wa kawaida, wanafanya kwa kuzidi mipaka ambayo Mungu amempa mwanadamu, maana yake wanatumia isivyo (mis-use) maumbile/ maungo ambayo Mungu amewapa.
Soma warumi 1:24-27. Sasa wao wanapofanya haya hawajui kwamba kuna hasara kubwa wanayoipata na wao wanafikiri ndio wanakwenda na dunia. Lengo la ujumbe huu ni kukueleza hasara za kufanya tendo la ndoa kabla ya ndoa nazo ni;

Thursday 27 November 2014

UBORA WA UTU WAKO

UBORA WA UTU WAKO

...Kwa sababu mtu akiwa ni msikiaji wa Neno tu, wala si mtendaji, mtu huyo ni kama mtu anayejiangalia uso wake katika kioo. Maana hujiangalia, kisha huenda zake, mara akasahau jinsi alivyo(Yakobo 1:22-24)

     Mstari wetu wa ufunguzi haujadili juu ya taswira, kwa maana ya umbo la nje au mwonekano wa mtu ajitizamaye katika kioo, bali ni "namna" au "aina" ya mtu. Mtendaji wa Neno hasahau "namna" yake alivyo; kiwango cha ubora wa utu wake.
    Utaelewa hilo vema endapo utasoma kuanzia mstari wa kumi na nane; inasema "Kwa kupenda Kwake Mwenyewe Alituzaa sisi kwa Neno la Kweli, tuwe kama limbuko la viumbe Vyake"(Yakobo 1:18).
     Mungu Alituzaa sisi kwa Neno la kweli; Ambalo ni, Injili ya Kristo, ili tuwe namna au aina ya uzao wa kwanza wa viumbe Wake. Hii ni ya kustaajabisha! Maana ya uzao wa kwanza ni nini? Inamaanisha wa kwanza na wa ubora wa juu kabisa wa viumbe wa Mungu.
     Ulipozaliwa mara ya pili, ukawa na aina ya ubora mpya wa maisha-maisha ya Mungu. 2 Wakorintho 5:17 inasema, " Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya." Kama kiumbe kipya ndani ya Kristo Yesu, wewe ni ukamilifu wa uzuri, na ubora wa juu kabisa wa kila kitu ambacho Mungu ameumba. Una nguvu dhidi ya shetani.
     Hivyo, Mkristo anaposema, "Nahitaji ukombozi dhidi ya shetani," ni kwa sababu amesahau "namna" na "aina" ya utu wake. Utahitaji vipi ukombozi dhidi ya shetani wakati wewe una nguvu zaidi yake?
     Biblia inasema umeketi pamoja na Kristo katika mbingu, juu zaidi ya mamlaka na nguvu zote. Upo katika mahala pa mamlaka ya juu kabisa ndani ya Kristo Yesu, juu sana ya shetani na kila kitu kinachohusiana naye.
     Fahamu ubora wa utu wako. Ndiyo maana tunakuletea Neno la Mungu kila siku kwa njia tofauti, kukupa nuru ya jinsi ulivyo ndani ya Kristo.

     Maombi
Baba Mpendwa, Nakushukuru kwa kunifanya wa kwanza na wa ubora wa juu katika vyote ulivyoviumba. Mimi ni utimilifu wa uzuri, wa mtindo wa ubora wa juu kabisa. Maisha yangu ni udhihirisho wa utukufu na ukuu wako; naonyesha ukamilifu wako na kudhihirisha hekima yako sura mbali mbali kwa ulimwengu, katika jina Lake Yesu. Amina

Soma Zaidi:
Warumi 6:4
Basi tulizikwa pamoja Naye kwa njia ya ubatizo katika mauti Yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.

Waefeso 2:10
Maana tu kazi Yake(kazi ya mikono yake), tuliumbwa tena katika Kristo Yesu, tuenende katika kazi njema, ambazo tokea awali Mungu aliziandaa ili tuenende kwazo.

MPANGO WA KUSOMA BIBLIA KWA MWAKA 1:
Waebrania 12:14-29
Ezekieli 13-15

MPANGO WA KUSOMA BIBLIA KWA MIAKA 2:
1 Yohana 3:1-12
Ezekieli 47.

HAKIKISHA UNASEMA SEHEMU YA "MAOMBI" AU "UKIRI" KWA SAUTI, USISEME MOYONI, KUNA UMUHIMU MKUBWA KATIKA KUSEMA.

NI KATIKA ROHO...SIO UFAHAMU

NI KATIKA ROHO...SIYO UFAHAMU.

Mungu ni Roho, nao wamwabuduo Yeye imewapasa kumwabudu katika Roho na kweli(Yohana 4:24)

     1 Wakorintho 2:14 inasema," Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni." Hii ni kwa sababu ukristo ni zaidi ya hisia! Ukosefu wa uelewa wa ukweli huu husababisha wengi kuchanganyikiwa katika kutembea kwao kiimani. Mungu huwasiliana na roho yako, si ufahamu wako. Imani huzalishwa katika roho na si katika ufahamu; ni mwitikio wa roho yako katika Neno la Mungu. Haihusiani kabisa na hisia zako.
     Hisia zetu hazikuumbwa ili kumhisi Mungu; Tunatembea Naye kutoka katika roho zetu; tunamtumikia kwa roho zetu, na kuelewa uhalisia wa mambo ya kiroho kwa kupitia roho. Fahamu zetu hazikuundwa kwa kazi hiyo; roho zetu tu ndizo zinaweza kuhusiana na Mungu. Kisha, kulingana na huo uhusiano, tunazipanga fahamu zetu kutokana na roho ili ziendane nayo, na kuongoza hisia zetu kutimiza kusudi letu.
     Hii inamaanisha, mwonekano tunaouonesha nje wakati wote unategemea hali ya roho zetu- jinsi tulivyo ndani.
     Ndiyo maana tunamuhitaji Roho Mtakatifu kutuongoza kwa kutokea ndani. Yeye pekee Ndiye Awezaye kufika ndani kabisa ya asili ya mwanadamu na kufanya mabadiliko ambayo Mungu huyataka kwetu- mabadiliko katika ukuaji na maendeleo-kutoka kiwango kimoja cha utukufu hadi kingine. Yeye pekee huweza kuongoza fahamu zetu kuwaza kwa kumwelekea Mungu, kufikiri kama Mungu, na kufikiri kutoka kwa Mungu.

  Maombi
Baba Mpendwa, nakushukuru kwa kuniongoza kwa Roho wako, kufikiri kama Wewe, na kuona mambo kwa mtazamo wako, na siyo tu katika mtazamo wa kibinadamu. Kadri nitembeavyo katika nuru ya Neno Lako, napata uzoefu wa ukuaji wa kipekee kutoka utukufu hadi utukufu, katika jina la Yesu. Amina.

Somo Zaidi:
Warumi 12:2
Wala msifwatishe namna ya dunia hii; bali mkageuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.

Waefeso 4:23-24
..na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu; mkavae utu upya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli.

MPANGO WA KUSOMA BIBLIA KWA MWAKA 1:
Yakobo 1
Ezekieli 17-19

MPANGO WA KUSOMA BIBLIA KWA MIAKA 2:
1 Yohana 4:1-14
Danieli 1-2.