Friday 10 November 2017

CHANGAMOTO ZA WAIMBAJI WA KIKE WA NYIMBO ZA INJILI


Kumekuwa na wimbi kubwa sana la waimbaji wakike wa nyimbo za injili,kila siku kwa wastani kuna waimbaji kumi wapya kabisa wanatambulishwa kwa njia mbalimbali aidha redioni,kwenye tv,magazetini,majaridani hata mitandaoni.
Wimbi hili la ongezeko la waimbaji wa kike haliendani na utoaji wa albamu. Katika hili kuna mijadala mbalimbali juu ya kwanini waimbaji wa kike wengi hawatoi albamu zao na hizi ndio baadhi ya sababu zinazochangia:

-          Mtaji – Waimbaji wengi hawana pesa (mtaji) kwa ajili ya kufanyia recordings ya nyimbo zao
-          Wito – Baadhi ya waimbaji hawana wito wa kumtumikia Mungu kwa njia ya uimbaji hivyo wanaimba tu kwa sababu wanajua kuimba wakisahau kuwa uimbaji ni huduma moja wapo katika huduma za kumtumikia Mungu na Mungu huwa hachezewi hivyo Mungu anaziba njia
-          Malengo – Kuna wengine wanaingia kwenye huduma hii kwa kutamani tu bila kuwa na malengo
-          Tamaa – Pia tama za kimwili kwa waimbaji na watengenezaji muziki (Producers) hupelekea kwa kukwamisha kazi kwa sababu baadhi huingia kwenye mahusiano ya kingono kitu ambacho hupelekea kupoteza concentration kwenye kazi pia dhambi huwa katikati yao.
-          Menejimenti – Waimbaji wengi hawana watu wa kuwasaidia kusimamia kazi zao ili waweze kuzifanyikisha ziweze kuifikia jamii kwa wakati muafaka.
HITIMISHO – Inahitajika kumuomba Mungu sana juu ya waimbaji maana ndio huduma inayopigwa vita sana na Shetani.

Credits to @THE BULLETS NEWS a whatsapp group 

No comments:

Post a Comment