Saturday 23 January 2016

UNAITWA,TUPA VAZI LAKO


MARKO 10;46-52
Inaelezea kulikuwa na Bartimayo kipofu alikuwa amekaa chini kando ya njia hajui maisha yake yatakuwaje,anavizia watu waje wamsaidie amekuwa ombaomba kwa miaka mingi kutokana na upofu wake,inawezekana nawe una upofu wa ndani umeteseka kwa jambo Fulani kwa miaka mingi hujui utatokaje hapo ktk magumu yako..YESU alipopita Bartimayo hakulaza damu akaanza kupaza sauti akimwita YESU...
Mstari 48-50. Na wengi wakamkemea ili anyamaze, lakini alizidi kupaza sauti, Mwana wa Daudi, unirehemu.Yesu akasimama akasema, Mwiteni. Wakamwita yule kipofu, wakamwambia, Jipe moyo; inuka, anakuita.AKATUPA VAZI

NAMNA YA KUWATAMBUA MANABII WA UONGO.

Bwana Yesu alishatuonya tujihadhari na manabii wa uongo na tena akawafananisha na mbwa mwitu wakali waliovaa ngozi ya kondoo (Math 7:15-23). Yesu alibainisha wazi kuwa namna pekee ya kuwatambua ni kuyachunguza matunda yao..Lakini mtume Petro amerahisisha zaidi kwa kufafanua tabia zao ktk 2Pet 2:1-22.,Nazo ni...

HASARA ZA KUFANYA NGONO KABLA YA NDOA.

Nimeitoa mahali naamini itakusaidia kijana
Andiko la Msingi ni Mithali 5:1-20
"Mungu ndiye aliyewaumba mtu mume na mtu mke, akawaweka bustanini ili wamtumikie. Mungu akamuumba mwanadamu na kumpa viungo mbalimbali katika mwili. Akawapa wanadamu maungo maalumu kwa ajili ya tendo la ndoa na kisha akaliweka tendo la ndoa kuwa takatifu, tena la halali kwa wanandoa tu, tena hasa wale waliounganishwa na yeye."
Sasa katika kizazi cha leo tunaona watu wengi hasa vijana ambao bado hawajaoana (kwa maana ya kuwa wanandoa) vijana hao wanafanya tendo hilo la ndoa (ngono) tena kwa uchafu usio wa kawaida, wanafanya kwa kuzidi mipaka ambayo Mungu amempa mwanadamu, maana yake wanatumia isivyo (mis-use) maumbile/ maungo ambayo Mungu amewapa.
Soma warumi 1:24-27. Sasa wao wanapofanya haya hawajui kwamba kuna hasara kubwa wanayoipata na wao wanafikiri ndio wanakwenda na dunia. Lengo la ujumbe huu ni kukueleza hasara za kufanya tendo la ndoa kabla ya ndoa nazo ni;