Na Mwandishi Wetu
Katika ulimwengu wa muziki wa Injili, tunashuhudia mambo mawili makubwa: wasanii wanaoamka kila siku na ndoto ya kumtumikia Mungu kupitia vipaji vyao, na jamii ya mashabiki ambao wanapaswa kuwa nguzo ya kuwaunga mkono. Hata hivyo, mwimbaji wa Injili @peter_lubango ametoa kilio cha dhati kuhusu namna ambavyo mashabiki na hata baadhi ya wasanii wenzao wanavyozembea kuthamini mchango wa wale wanaobeba ujumbe wa wokovu.
