Friday, 19 September 2025

THAMANI YA KUMSHIKA MSANII WA INJILI MKONO WAKIWA HAI

Na Mwandishi Wetu

Katika ulimwengu wa muziki wa Injili, tunashuhudia mambo mawili makubwa: wasanii wanaoamka kila siku na ndoto ya kumtumikia Mungu kupitia vipaji vyao, na jamii ya mashabiki ambao wanapaswa kuwa nguzo ya kuwaunga mkono. Hata hivyo, mwimbaji wa Injili @peter_lubango ametoa kilio cha dhati kuhusu namna ambavyo mashabiki na hata baadhi ya wasanii wenzao wanavyozembea kuthamini mchango wa wale wanaobeba ujumbe wa wokovu.

Friday, 10 November 2017

CHANGAMOTO ZA WAIMBAJI WA KIKE WA NYIMBO ZA INJILI


Kumekuwa na wimbi kubwa sana la waimbaji wakike wa nyimbo za injili,kila siku kwa wastani kuna waimbaji kumi wapya kabisa wanatambulishwa kwa njia mbalimbali aidha redioni,kwenye tv,magazetini,majaridani hata mitandaoni.
Wimbi hili la ongezeko la waimbaji wa kike haliendani na utoaji wa albamu. Katika hili kuna mijadala mbalimbali juu ya kwanini waimbaji wa kike wengi hawatoi albamu zao na hizi ndio baadhi ya sababu zinazochangia:

Saturday, 23 January 2016

UNAITWA,TUPA VAZI LAKO


MARKO 10;46-52
Inaelezea kulikuwa na Bartimayo kipofu alikuwa amekaa chini kando ya njia hajui maisha yake yatakuwaje,anavizia watu waje wamsaidie amekuwa ombaomba kwa miaka mingi kutokana na upofu wake,inawezekana nawe una upofu wa ndani umeteseka kwa jambo Fulani kwa miaka mingi hujui utatokaje hapo ktk magumu yako..YESU alipopita Bartimayo hakulaza damu akaanza kupaza sauti akimwita YESU...
Mstari 48-50. Na wengi wakamkemea ili anyamaze, lakini alizidi kupaza sauti, Mwana wa Daudi, unirehemu.Yesu akasimama akasema, Mwiteni. Wakamwita yule kipofu, wakamwambia, Jipe moyo; inuka, anakuita.AKATUPA VAZI

NAMNA YA KUWATAMBUA MANABII WA UONGO.

Bwana Yesu alishatuonya tujihadhari na manabii wa uongo na tena akawafananisha na mbwa mwitu wakali waliovaa ngozi ya kondoo (Math 7:15-23). Yesu alibainisha wazi kuwa namna pekee ya kuwatambua ni kuyachunguza matunda yao..Lakini mtume Petro amerahisisha zaidi kwa kufafanua tabia zao ktk 2Pet 2:1-22.,Nazo ni...

HASARA ZA KUFANYA NGONO KABLA YA NDOA.

Nimeitoa mahali naamini itakusaidia kijana
Andiko la Msingi ni Mithali 5:1-20
"Mungu ndiye aliyewaumba mtu mume na mtu mke, akawaweka bustanini ili wamtumikie. Mungu akamuumba mwanadamu na kumpa viungo mbalimbali katika mwili. Akawapa wanadamu maungo maalumu kwa ajili ya tendo la ndoa na kisha akaliweka tendo la ndoa kuwa takatifu, tena la halali kwa wanandoa tu, tena hasa wale waliounganishwa na yeye."
Sasa katika kizazi cha leo tunaona watu wengi hasa vijana ambao bado hawajaoana (kwa maana ya kuwa wanandoa) vijana hao wanafanya tendo hilo la ndoa (ngono) tena kwa uchafu usio wa kawaida, wanafanya kwa kuzidi mipaka ambayo Mungu amempa mwanadamu, maana yake wanatumia isivyo (mis-use) maumbile/ maungo ambayo Mungu amewapa.
Soma warumi 1:24-27. Sasa wao wanapofanya haya hawajui kwamba kuna hasara kubwa wanayoipata na wao wanafikiri ndio wanakwenda na dunia. Lengo la ujumbe huu ni kukueleza hasara za kufanya tendo la ndoa kabla ya ndoa nazo ni;

Thursday, 27 November 2014

UBORA WA UTU WAKO

UBORA WA UTU WAKO

...Kwa sababu mtu akiwa ni msikiaji wa Neno tu, wala si mtendaji, mtu huyo ni kama mtu anayejiangalia uso wake katika kioo. Maana hujiangalia, kisha huenda zake, mara akasahau jinsi alivyo(Yakobo 1:22-24)

     Mstari wetu wa ufunguzi haujadili juu ya taswira, kwa maana ya umbo la nje au mwonekano wa mtu ajitizamaye katika kioo, bali ni "namna" au "aina" ya mtu. Mtendaji wa Neno hasahau "namna" yake alivyo; kiwango cha ubora wa utu wake.
    Utaelewa hilo vema endapo utasoma kuanzia mstari wa kumi na nane; inasema "Kwa kupenda Kwake Mwenyewe Alituzaa sisi kwa Neno la Kweli, tuwe kama limbuko la viumbe Vyake"(Yakobo 1:18).
     Mungu Alituzaa sisi kwa Neno la kweli; Ambalo ni, Injili ya Kristo, ili tuwe namna au aina ya uzao wa kwanza wa viumbe Wake. Hii ni ya kustaajabisha! Maana ya uzao wa kwanza ni nini? Inamaanisha wa kwanza na wa ubora wa juu kabisa wa viumbe wa Mungu.
     Ulipozaliwa mara ya pili, ukawa na aina ya ubora mpya wa maisha-maisha ya Mungu. 2 Wakorintho 5:17 inasema, " Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya." Kama kiumbe kipya ndani ya Kristo Yesu, wewe ni ukamilifu wa uzuri, na ubora wa juu kabisa wa kila kitu ambacho Mungu ameumba. Una nguvu dhidi ya shetani.
     Hivyo, Mkristo anaposema, "Nahitaji ukombozi dhidi ya shetani," ni kwa sababu amesahau "namna" na "aina" ya utu wake. Utahitaji vipi ukombozi dhidi ya shetani wakati wewe una nguvu zaidi yake?
     Biblia inasema umeketi pamoja na Kristo katika mbingu, juu zaidi ya mamlaka na nguvu zote. Upo katika mahala pa mamlaka ya juu kabisa ndani ya Kristo Yesu, juu sana ya shetani na kila kitu kinachohusiana naye.
     Fahamu ubora wa utu wako. Ndiyo maana tunakuletea Neno la Mungu kila siku kwa njia tofauti, kukupa nuru ya jinsi ulivyo ndani ya Kristo.

     Maombi
Baba Mpendwa, Nakushukuru kwa kunifanya wa kwanza na wa ubora wa juu katika vyote ulivyoviumba. Mimi ni utimilifu wa uzuri, wa mtindo wa ubora wa juu kabisa. Maisha yangu ni udhihirisho wa utukufu na ukuu wako; naonyesha ukamilifu wako na kudhihirisha hekima yako sura mbali mbali kwa ulimwengu, katika jina Lake Yesu. Amina

Soma Zaidi:
Warumi 6:4
Basi tulizikwa pamoja Naye kwa njia ya ubatizo katika mauti Yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.

Waefeso 2:10
Maana tu kazi Yake(kazi ya mikono yake), tuliumbwa tena katika Kristo Yesu, tuenende katika kazi njema, ambazo tokea awali Mungu aliziandaa ili tuenende kwazo.

MPANGO WA KUSOMA BIBLIA KWA MWAKA 1:
Waebrania 12:14-29
Ezekieli 13-15

MPANGO WA KUSOMA BIBLIA KWA MIAKA 2:
1 Yohana 3:1-12
Ezekieli 47.

HAKIKISHA UNASEMA SEHEMU YA "MAOMBI" AU "UKIRI" KWA SAUTI, USISEME MOYONI, KUNA UMUHIMU MKUBWA KATIKA KUSEMA.